Скачать книгу

zilifunikwa kabisa na magamba. Nyuzo zao ambazo nusu zilikuwa na umbo la duaradufu zingenyooka nje kutoka maskio na kuchukua umbo la nusu kengele. Hawakuwa na mashavu yoyote na mapua yao yaliyokuwa kama nyoka na hayakuonekana kabisa. Walikuwa wakali, lakini hawakuwa werevu hasa, walikuwa kabila pekee ambalo lingengangania mamlaka na Wa-aniki kwa idadi na nguvu. Walivaa koti refu la kiuno la hariri ambalo linafunikwa na miguu yao na ambayo inafungwa kwa vifungo kwenye kifua. Ili kupata usaidizi wao, Ruegra alikuwa amemteua mmoja wao kuwa Gavana wa Bonobo.

      Jenarali alikaribishwa kwa utukufu kwenye ukumbi wa glasi kwenye jengo la serikali, ambako kuna mazingira mazuri ya kitropiki ya kupendeza. Ulikuwa usiku wa kustaajabisha na anga ilikuwa imewashwa kwa akisi wa miviringo hiyo.

      Ruegra alikuwa akitazama kupitia glasi iliyokuwa ikiakisi picha yake.

      Rangi ya mwili wake thabiti, iliyokuwa imefunikwa na ngozi kavu, ambazo zingebadilisha rangi kulingana na mazingira. Sura haikuweza kutambulika kati ya miti iliyo nje. Taji ngumu iliyotengenezwa kwa tishu za karatini na ilikuwa na urefu wa Kudus 30 au inchi 11 ilikuwa imepamba sura yake, kuanzia kichwa. Taji hiyo ingefunguka kama kuna hatari na inakuwa silaha ambayo Wa-Aniki walitumia wakati wa mwanzo wa utawala wake kumtisha adui. Inapofunguliwa kwenye mkono, ingetumika kama ngao.

      Kutokana na uso wake wa mviringo ngozi kavu zingesinyaa na kuwa sawa kwa rangi. Chini ya paja la uso wake, nyusi na kobe zake za bluu za karatini hufanya macho yake kubwa ya kijani kibichi na mashavu yake laini yenye rangi yaliyodhihirika. Pua lake kubwa lililolemaa, kama la bondia, lilihitiliafiana na sura yake. Mdomo wake uliwiana vizuri: mdomo wake wa kijani ulikuwa kubwa na nono.

      Waaniki walikuwa wakubwa zaidi kwa urefu miongoni mwa watu wote katika mfumo wa jua na sayari zake na kwa sababu hiyo daima wamekuwa juu katika piramidi ya Wanyama wawindaji.

      Sawa na Wa-aniki, Ruegra kwa kawaida huvaa sketi iliyona vipande viwili vilivyopasuliwa ambavyo vingeonesha Ngozi kavu kwenye mwilini wake. Begani angevaa rasi, ambayo inadhamiriwa kuonesha tabaka na majukumu yake. Rasi yake ilikuwa na rangi ya dhahabu, ilioashiria cheo chake cha amri na ilipambwa na sura ya rangi ya moshi-kijivu na nakshi ya rangi sawa ilioonesha ndege ya uwindaji wa Atrex.

      "Ninasalimu asiyeweza kushindwa miongoni mwa watu wa Carimea. Unakaribishwa kila wakati katika nchi yetu, jenarali wangu. Safari ilikuwaje?" akamsalimu Mastigo kwa kumwinamia kidogo.

      "Ilikuwa nzuri. Ujumbe unaendelea kwa njia nzuri." Ruegra akadanganya. "Nahitaji tu kupumzika. Pete hizo za sayari hufanya meli ya angani kutetemeka kidogo." Alisema ili aachane na mzungumzaji.

      Mastigo alimpa kinywaji cha matunda ya huko ili aburudike baada ya safari ndefu baina ya sayari. Ilikuwa afadhali kwa Jenerali kuketi kwani alihitajika kuripoti tukio lisilo la kawaida.

      "Ninatukio lisilo la kawaida ambalo linahitaji kuwasilishwa kwako. "Siku mbili zilizopita za Bonobo, tuliona chombo cha angani cha biashara kilipokuwa kikiingia eneo letu bila ruhusa. Walinzi hawakuweza kuisimamisha kwa wakati ufaao. Kwa hivyo, ilitumbukia katika Bahari ya Unyamavu kabla hatujatathmini hatari zake halisi.

      Tumefanya utafiti na tumepata kwamba mmiliki amekiuza kwa mwanamke mmoja wa Eumenide. Nimetuma askari kadhaa wa doria kuchunguza eneo linalodaiwa kutua. Lakini kama unavyojua, haiwezekani kupokea mawasiliano ya aina yoyote kutoka Bahari ya Unyamavu. Kwa hiyo, tunachotakiwa kufanya ni kusubiri."

      Ruegra alikasirishwa na jinsi Gavana alivyoshikilia ukweli huo usio na maana na akauliza:

      "Ni nini cha ajabu kuhusu hayo? Sielewi..."

      "Angalia mahali ilikuwa inaelekea..." akasema Mastigo akionesha ramani ya Bahari ya Unyamavu.

      "Hapa ndiko mahali ngome takatifu ya Bonobo inapopatikana..." Ruegra akanong’oneza.

      "Ndio sababu nilichukua huru wa kuripoti tukio dogo kama hilo. Nimetuma timu kuchunguza eneo hilo. Inaweza kuwa ililingana tu, lakini ni heri kuwa salama kuliko kusema pole. Mahali hapo pamejaa miujiza. Ingekuwa makao makuu mazuri kuanzia migogoro, ukizingatia ukosefu wa mawasiliano na ishara za rada. Ni kama shimo jeusi.

      "Unaweza kuwa sahihi. Endelea kunisasisha, Mastigo. Sasa ni bora ikiwa nitapumzika. Kesho tutaondoka alfajiri."

      Usiku huo Ruegra alikuwa na vitu vingine vya kufikiria. Baada ya kurudi chumbani kwake, aliketi kwenye sofa laini na kujipatia kinywaji aina ya Sidibé, pombe kali ya kienyeji inayopatikana kwa cacti. Alikuwa akitazama angani huku fikra zake zikikimbizana kama mawimbi kabla ya dhoruba.

      Safari ambayo alikuwa tu amemaliza imekuwa ya janga kabisa, kinyume na kile alichokuwa amemwambia mshirika wake anayemwamini.

      Alikuwa amezuru Mwezi wa sayari ya Enas, haswa kwa koloni ya uchimbaji madini ya Stoneblack, kambi ndogo inayofahamika sana kwa marumaru yake. Jenarali huyo alikuwa akihitajika kukutana na mtu ambaye babaye mwenyewe alikuwa anamheshimu sana: adui wa zamani wa Carimea.

      Koloni hiyo ilitawaliwa na kabila la Triki. Walikuwa watu kutoka Carimea, kama Wa-aniki, lakini walikuwa na ushawishi wa pili kwenye usimamizi wa sayari hiyo.

      Walikuwa wamejitolea kuhudumu, lakini hawaaminiki. Walikuwa wamejidhihirisha kuwa wasaliti mara tu upepo unapobadilisha mwelekeo. Hata rafiki zake mwenyewe wangeweza kupanga njama dhidi yake kwenye Mwezi huo. Kwa hivyo, ilibidi kufanya ukaguzi huo uonekane kama ziara ya ghafula akiwa na nia ya kurudisha baadhi ya visukuu vya mwezi kwa nduguye wakati wa kurudi.

      Ruegra alitembea mbele ya maafisa hao. Alileta kiwiko chake karibu na bega lake na huku mkono wake ukiwa sambamba na sakafu na karibu na kinywa chake, akawasalimia. Ishara hiyo ilionesha ukimya mbele ya amri yake pamoja na utii kamili. Walikuwa bado wamenyamaza mbele yake.

      Koloni hiyo ya uchimbaji madini iliajiriwa kama wahalifu wanaofanya kazi ya lazima na wafungwa wa kivita kufanya kazi kwa gharama rahisi. Walinzi hao wangemlinda mtumwa mmoja hasa...Alikuwa mtu wa Ruegra. Sio tu kwamba alikuwa mtumwa wa kiwango cha juu, lakini pia alikuwa amepata heshima kutoka kwa watumwa wenzake na aliweza kuwaakilisha.

      Jenarali huyo, aliyeandamana na nahodha na kufuatiwa na wanajeshi, aliwekwa kwenye chumba cha kupumzika na cha kutolea amri, amchacho kilikuwa kimetengewa afisa huyo.

      Nahodha huyo alitoa heshima zake na kuuliza iwapo angetaka kitu.

      Ruegra hakupoteza wakati wowote. Alikataa ofa hiyo na akaamuru:

      "Ninataka kuthibitisha hali ya wafungwa wa kisiasa ambao walichukuliwa wakati wa vita dhidi ya Sayari ya Sita. Wacha niongee na afisa mwenye cheo cha juu."

      "Jenarali Wof?"

      "Ndio, haswa. Mlete kwangu. " "

      "Ndio, bwana."

      Kamanda akaguna kwa walinzi na dakika chache baadaye walirudi chumbani akiandamana na mtu wa makamo. Alionekana mchovu na kukosa nguvu, lakini bado alikuwa na kiburi na sura ya mpiganaji asiye na hofu.

      "Tuacheni." akamrishwa Ruegra.

      Alisalia pekee akiwa na adui mwenye akili kali. Alikumbuka kuwa wakati wa vita alikuwa ameweza kubadilisha hali mbaya ambayo ilikuwa imetabiri kifo chake, shukran kwa kufikiria kimkakati na licha ya kuwa na watu wachache kutoka Sayari ya sita chini ya utawala wake.

      Alisita kwa sekunde kadhaa kabla ya kuzungumza. Alikuwa tayari amewaza kuhusu mikakati kadhaa wakati wa safari yake. Alijua kwamba haingewezekana kumshika adui yake bila kufahamu. Ilikuwa wakati wa kuchukua mmoja na kuanza makabiliano.

      Aliamua kuendelea na ibada hiyo ya kumsifu akitarajia kwamba uzee wake na uchovu wake umemfanya kudhoofika zaidi.

      "Nakusalimu, Wof. Ninaweza kusema kwamba hauonekani vibaya licha ya kutopewa matibabu bora. Hata hivyo nimeamrisha upatiwe vitabu na elimu. " "

      "Muda mrefu sijakuona." alisema Wof, akimtazama jenarali huyo na macho yake ya kina na meusi. "Ni nini kilikuleta mahali hapa ambako imesahaulika na mwangaza, ambako giza inatawala?"

      "Nilikuja hapa kuongea nawe kuhusu baba yangu. Nakumbuka kuwa nikiwa mtoto angefikria kuhusu Ngozi ambayo ulijua siri zote kuihusu. Sasa kwa kuwa ninazeeka, wakati mwingine ninafikiria kumhusu na kushangaa iwapo kuna ukweli kuhusu hadithi hiyo."

      Wof alijaribu kuficha ushangao wake kwa kupapasa nywele zake hizo ambazo zilikuwa zinampa

Скачать книгу